Home » » "BILA KUSOMA VITABU, KANISA LITAPATA UTAPIAMLO" PR. ROBERT TUVAKO

"BILA KUSOMA VITABU, KANISA LITAPATA UTAPIAMLO" PR. ROBERT TUVAKO

Written By SHINYANGA CENTRAL SDA CHURCH on Monday, July 31, 2017 | July 31, 2017


Kisa cha kwanza: Palikuwepo na mfungwa mmoja aliulizwa, “Chakula cha mwisho unachopenda kula ni kipi? Na wakati huo kamera ziliendelea kuonyesha tukio hilo. Aliagiza alichopenda na camera ziliendelea kuonyesha akila chakula hicho na wakati huo huo tena kamera zilihamia kwa familia zilizoathirika na matendo mabaya ya mfungwa huyu na vile vile kamera ilihamia kuonyesha familia ya mfungwa huyu. Cha ajabu kauli yake ya mwisho haikuwa na majuto bali aliendelea kusisitiza kuwa alitenda hayo yote kwa makusudi.

Kisa cha pili: Costen Fleming mwenye miaka 75, aliugua kwa kupasuka mishipa ya damu na aliambiwa kuwa hatapona. Aliambiwa unataka nini kabla hujafa? Huyu aliomba sigara na wine

Leo ukiambia unataka nini kabla ya kufa utaomba nini? Na sasa ninanena na wewe unayesoma ujumbe huu, ungekuwa wewe ungeomba nini? Unavyojenga moyo wako ndivyo unavyojenga tabia yako, na hicho kilicho katika moyo wako ndicho kitaonekana mara ya mwisho katika wakati wako wa mwisho. Ukubwa wa tabia unaweza kuonekana hata katika  dakika ya mwisho.

Kamwe sio bure kuhudhuria mikutano ya kiroho. Kiini cha somo kinapatikana katika aya 13 ya 2 Timotheo 4, ambapo tunasoma Mtume Paulo anamwandikia Timotheo, na hii ndio sura  ya mwisho ya mtume Paulo aliyoandika na kana kwamba Mtume Paulo alijua ndio mwisho wake. Tunajifunza kuwa ulikuwa ni wakati za mwisho kwa mtume Paulo na alianza kwa kuagiza kazi zilizo katika moyo wake. 

Paulo aliyekuwa Sauli alikuwa mtu maarufu sana, mwenye uwezo, alikuwa akiheshimika sana, na ni tajiri sana. Na Yesu alipokutana naye hakuwa peke yake katika msafara wake maana alikuwa ni mtu mashuhuri sana katika jamii yake.
Lakini Yesu alipomtawala  Paulo, Paulo alianza kugawa kila utajiri aliokuwa nao. Na wimbo wake ulikuwa ni injili ya Yesu. Na alipokuwa gerezani aliagiza vitu viwili tu, Hakuagiza dhahabu wala almasi.
 Kwaya ya Kanisa la Waadventista wa Sabato Kirumba-Mwanza wakiimba wakati wa Ibada

Mara kadhaa Imani yetu haifanani kama tulivyokuja kwa Yesu, maana tupo tunaokuja kwa Yesu tukiwa ni maarufu na wakati Fulani wengine twaja tukiwa maskini. Vyovyote tunavyokuja, kwa mali au kwa umaskini, iwe kwa hadhi au dharau, ninapenda kutoa  wito kwako mpendwa umalize wito wako wa hapa duniani na Yesu Kristo. Ni heri makombo Yesu Kristo kuliko keki za Shetani.

Ombi la kwanza ni Joho. Kwa nini Paulo aliomba Joho? Tazama Paulo yuko kwenye shimo gerezani, kuna baridi kali sana katika shimo hilo ambalo lina unyevu kila wakati. Wakati alipokamatwa, alimpa Karpo vitu viwili ili visije vikapotea, alimpa joho na vitabu. Katika gereza Paulo hana hata mtu wa kumuomba joho. Aliagiza joho lake. “kilicho chako kina thamani kuliko vya wengine”.

Sijui kama mimi na wewe kama tungepewa fursa ya kuagiza sijui tungeagiza nini? Paulo aliagiza Joho lake, alijua kwamba hata kama atakufa, mwili wake utakuwa umefunikwa na joho lake. Ndiye aliyeandika kuwa mwili huu ni hekalu la Mungu. Aliendelea kuwajibika katika mwili wake.

Ombi la pili ni vitabu. Kwa nini vitabu? Kwa ulimwengu wa sasa katika basin a usafiri mwingine wengi utawakuta wana simu wakichati. Lakini pia katika karne iliyopita katika magari ya abiria, tuliwashuhudia watu wakizungumza. Na katika nchi za magharibi utakuwa wasafiri wengi wanasoma vitabu mbalimbali wakiwa ndani ya vyombo vyao vya usafiri.
Mpendwa msomaji, napenda kuwapatia ujumbe huu kuwa, Kando ya torati, Mtume Paulo alipenda kusoma vitabu vingine (Matendo 17:28 “Kwa maana ndani yake tunaishi, tunakwenda, na kuwa na uhai wetu. Kama vile mmoja wenu, mtunga mashairi alivyosema, maana sisi sote tu wazao wake”)

Paulo anamwandikia Timotheo kuomba mambo makuu mawili na hasa jambo la pili kwa sababu anajua kuwa atakaponyongwa atakuwa amemwachia ujumbe kuwa bila kusoma vitabu, kanisa litapata utapiamlo. Changamoto zetu ni kufundishana kupitia usomaji wa vitabu. Sisemi kusoma tu kesha la asubuhi, bali ninachomaanisha ni usomaji wa vitabu wa kutafuta hekima ya mbinguni ipambanuayo mambo kwa hekima kuu. Bwana anataka kanisa linalosoma. Heri asomaye. 

BWANA AKUBARIKI
Share this article :

Post a Comment

 
Need Support? Contact : Creating Website and Blog | Stanley Isaac Manyonyi | Twitter
Copyright © 2017. SHINYANGA CENTRAL SDA CHURCH - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger