Home » » IBADA YA KUFUNGUA SABATO

IBADA YA KUFUNGUA SABATO

Written By SHINYANGA CENTRAL SDA CHURCH on Friday, March 31, 2017 | March 31, 2017

Ruth Ng'washi (Mrs Maeja)
    WIMBO: NAMBA 125-Uniangalie atwambia Yesu aliyetufia

"Tukiwa tunajiandaa na meza ya Bwana Jumamosi tarehe 01 April 2017, tujitathimini katika kitabu cha Zaburi 14:2 ambapo tunapata ujumbe wa jinsi Mungu anatuona. Wote tunahesabika ni wadhambi lakini kupitia kifo cha Yesu kristo kila mmoja amepata nafasi ya kurithi Ufalme wa Mungu.

Tunapo tafakari kwa muda wa juma hili, tutagundua kuwa muda mwingi tumeutumia kutafuta pesa. Neno la Bwana siku ya leo linatufundisha kumtafuta Mungu kwa bidii. Tutakapomtafuta Mungu kwa bidii, mambo mengine atatupatia.

Sote kama wadhambi tunaleta toba yetu kwa Mungu mwenye huruma na upendo. Tunapoomba toba mungu wetu mwaminifu hutupatia nafasi nyingine ya kipekee zaidi ya kuujua ukuu wake. kwa kutafakari mambo ambayo hayako sawa kutasaidia kuomba msamaha kwa Mungu wetu. Kila mmoja wetu aombe toba binafsi ya kupata kibali ili ibada yetu ya Meza ya Bwana ipokelewe kwa utukufu wa Mungu."

BWANA ATUBARIKI SOTE




Share this article :

+ comments + 1 comments

21 February 2020 at 13:13

Ubarikiwe na bwana

Post a Comment

 
Need Support? Contact : Creating Website and Blog | Stanley Isaac Manyonyi | Twitter
Copyright © 2017. SHINYANGA CENTRAL SDA CHURCH - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger