Home » » JIANDAE KUKUTANA NA YESU KATIKA MAKAMBI 2017

JIANDAE KUKUTANA NA YESU KATIKA MAKAMBI 2017

Written By SHINYANGA CENTRAL SDA CHURCH on Monday, July 17, 2017 | July 17, 2017

Mchungaji Simeo Makunja- Mkurugenzi wa Kaya na Familia na Katibu wa Wachungaji wa Jimbo la Nyanza Kusini

 Mkurugenzi kutoka Jimbo la Nyanza Kusini anayesimamia masuala ya Kaya na Familia ambaye pia ni Katibu wa Wachungaji wa Jimbo amesema kuwa Yesu Kristo alikuwepo toka mwanzo wa uumbaji wa Dunia, kwa hiyo wanadamu wote wasikatae mafundisho ya Yesu ili wapate hekima. "Ana heri mtu asikiaye neno la Mungu naye atapata kibali mbele za Mungu. Na kila achukiaye hekima ya Mungu anakaribisha mauti na kupotea milele". Amesema Mchungaji Makunja.

Mchungaji Makunja amesema hayo wakati wa usiku akifundisha neno la Mungu katika kipindi cha "Wazo la Usiku". Akinukuu maneno katika kitabu cha Yohana 1:14 amesema kuwa kupitia Yesu Kristo, Mungu wa Mbinguni amejifunua na sasa sio siri. Kupitia Yesu Kristo ukombozi wa mwanadamu ulitimia na kumfanya mwanadamu awe huru katika uchaguzi wa kumtumikia Mungu au Shetani.

Pia Mchungaji Makunja amemuelezea Yesu Kristo Ni Mungu ambaye kupitia kwake kila kiumbe chenye uhai na visivyo hai viliumbwa kupitia kwake na kupitia kwake Yesu Kristo, Upendo wa Mungu umeonekana kupitia Kifo cha Yesu.

Mchungaji Makunja ametoa wito wa kuhudhuria sikukuu ya vibanda ili kila atakayehudhuria apate hekima ya Yesu Kristo na kuweza kupata kibali katika Ufalme wake ambao ameenda kuundaa mbinguni. Amesema uamuzi wa Yesu Kristo kufanyika Mwanadamu ilikuwa na kusudi la Kuumba na ukombozi wa Mwanadamu ili mwanadamu aweze kumwabudu na Kumsuduju Yesu Kristo (Ufunuo 13:8-9). "Tunapokuja hapa kwenye makambi, tunakuja kutafuta hekima na kuweza kumwabudu Yesu wetu ambaye ndiye Mungu wetu".


Share this article :

Post a Comment

 
Need Support? Contact : Creating Website and Blog | Stanley Isaac Manyonyi | Twitter
Copyright © 2017. SHINYANGA CENTRAL SDA CHURCH - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger