Pale Roho wa Kristo anapokaa ndani ya moyo wa mume na mke, ndoa yao inaweza kuwa mvuto mkubwa wa kujenga maisha ya watoto wao na kuwaongoza kuelekea kwenye maadili chanya.
Waefeso 5:25, Tito 2:4 na Kumbukumbu la Torati 6:6-7
Kwa sababu neema ya Kristo inauwezo wa kuimarisha na kuboresha kile ambacho Shetani alichokiharibu katika ndoa takatifu. Ni nini umuhimu wa ndoa ya Kikristo kwa mafundisho na maisha ya watoto?
Katika familia yenye wazazi wawili mahusiano mazuri ya wazazi yana mvuto kwa watoto na hujenga kuimarisha mahusiano ya watoto wao kwao, wazazi kwa watoto na watoto kwa jamii nzima. Upendo wa wazazi unafananishwa na mfumo wa joto nzuri ndani ya nyumba ambapo watoto hawatasikia baridi.
Matendo yanayostawisha upendo ni yapi?
1. Maneno yenye upendo na shukrani
2. Ujumbe unaondikwa kwa wenzi na kusomwa mbele ya watoto.
3. Kupeana Zawadi kwa wenzi
Kutokuheshimiana kwa wazazi kuna athiri kwa kiasi kikubwa ukuaji wa watoto kimaadili. Huchangia kwa asilimia kubwa kizazi cha watoto hao kutokuwa na ndoa yenye manufaa wakati watakapokuwa tayari kuingia katika taasisi yao ya ndoa.
Post a Comment