Home » » KUALIKWA KATIKA KARAMU

KUALIKWA KATIKA KARAMU

Written By SHINYANGA CENTRAL SDA CHURCH on Sunday, April 16, 2017 | April 16, 2017




 
WAZO KUU
Zawadi aliyotoa Yesu Kristo katika karamu ya harusi kule Kana ilikuwa ni ishara ya kile anachotaka kutufanyia katika ndoa zetu.

Fungu kuu:
Yohana 2:1-12

Baada ya divai nzuri, huja divai mbaya au kuisha kwa divai. Kisa hiki kinatupa siri kuu tatu katika ndoa.

1. Hakikisha unamwalika YESU katika ndoa zetu. Yeye ana uwezo wa kufanya kwa ubora wa juu.
2. Fanya kile anachokuambia
3. Toa vilivyo vyema zaidi.


Uzoefu na takwimu vinadhihirisha kwamba huu upungufu wa divai bahati mbaya hujitokeza katika ndoa nyingi hata leo. Sisi ni binadamu, hatuwezi kuishi bila ukomo wa rasilimali chache za kibinadamu tulizo nazo.

Matatizo yanaweza kuwa makubwa au madogo. Tofauti ya ndoa za Kikristo na zile za kidunia ni moja. Katika ndoa za Kikristo, Yesu ni wa kwanza katika orodha ya wageni.

Leo Yesu anataka kutupatia mahitaji yetu na kututatulia matatizo yetu. Naye anataka kufanya zaidi kuliko mipaka na matarajio ya kibinadamu. Fanya kila atakachokwambia.
Share this article :

Post a Comment

 
Need Support? Contact : Creating Website and Blog | Stanley Isaac Manyonyi | Twitter
Copyright © 2017. SHINYANGA CENTRAL SDA CHURCH - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger