Mkufunzi kutoka shule ya Waadventista Alpha iliyopo Kigoma, ndugu Kulu Jeremiah Mahwago alifundisha wanasemina faida ya kutumia matofali yanayotokana na udongo na saruji. Mojawapo ya faida ya matofali haya ni rafiki kwa mazingira kwa sababu hayahitaji matumizi ya nishati ya moto kama vile kuni kuyachoma.
Pia mkufunzi alikaririwa akisema katika ujenzi hutumia mfumo wa kupachika bila kutumia saruji au udongo. Mara baada ya kupachika na kufika katika hatua ya madirisha ndipo mjenzi atalaimika kutumia saruji kwa lengo la kufunga renta.
Uhai wa tofali hizi unategemea maji kwa siku 28 na hazitumii jua kukaushwa bali baada ya kufyatuliwa zinahitaji kivuli maana zinakauka kwa kutegemea upepo.
Mchungaji wa mtaa wa Shinyanga Mjini, mchungaji Kilinda J.J anashukuru uongozi wa jimbo la kusini mwa ziwa Victoria kuleta semina katika eneo la Ndala- Shinyanga. Amesema kuwa semina hii imewasaidia vijana wa kanisa kupata ujuzi wa kutengeneza matofali yatokanayo na saruji na udongo, kwa hiyo anaamini baada ya semina hii vijana watarudi katika maeneo yao na kuanza kujiajiri. Pia vijana wataweza kujenga nyumba makazi yao kwa gharama nafuu.
Wakati huo huo mkurugenzi wa elimu na uhuru wa dini wa jimbo la kusini mwa ziwa Victoria mwalimu Isaacks Manyonyi amesema Shinyanga Adventist Secondary School itaanza Januari 2018 na kuwaomba wadau wote wa elimu kutoa misaada ya hali na mali ili kuweza kukamilisha ujenzi wa shule hii.
Semina hii imeanza tarehe 10-13 April 2017
Post a Comment