Home » » WANANDOA KANISANI WALISHANA KEKI

WANANDOA KANISANI WALISHANA KEKI

Written By SHINYANGA CENTRAL SDA CHURCH on Saturday, April 22, 2017 | April 22, 2017

Mzee Kasonzo Washington akimlisha keki mke wake


FUNGU KUU:
“MPENZI NAOMBA UFANIKIWE KATIKA MAMBO YOTE NA KUWA NA AFYA YAKO, KAMA ILE ROHO YAKO IFANIKIWAVYO” 3 YOHANA 1:2 

Sabato ya leo iliabudiwa kwa kicho na kisha wanandoa waliohudhuria ibada walipata nafasi ya kulishana keki kama ishara ya kukumbuka tukio la siku walipoona. Ibada ya leo ilikuwa ni hitimisho la juma la kaya na familia ambalo somo kuu lilikuwa katika kuhamasisha wanandoa kuishi katika viapo vyao.


Ndugu Raphael na mke wake wakilishana keki
Ndugu Sarya na mke wake wakilishana keki

WAZO KUU

Mungu ametoa baadhi ya kanuni rahisi za kinga ambazo huweza kusaidia wanandoa kudumisha afya ya ndoa zao.

NI KWANINI NDOA INAHITAJI KINGA.
Hebu angalia mfano huu
1.       Mwana-sayansi mmoja aliwahi kusema kwa kila kijiko kimoja cha udongo wa bustani anakadiria kuwa kuna viumbe milioni 500
2.       Kwamba nusu kijiko cha mate kina bilioni moja ya viumbe visivyoonekana.

Wakati baadhi ya vijidudu na bakteria hawa wana madhara, lakini wengi wao hawana madhara.
Kuzungumzia mifano hiyo miwili mwandishi ametoa mfano wa kile wanachofanya wanaharusi kati nchi hizi za magharabi pale mchungaji  anapomwambia bwana harusu “ SASA UNAWEZA KUMBUSU BIBI HARUSI” Wenzi hao hushiriki zaid ya upendo. Wanachofanya ni kubadilishana majeshi mengi sana ya viumbe hai.
Ona hili. Tunaishi katika mazingira yenye uwadui na sisi kwa hali ya kimwili, kiroho na kimahusiano. Kirusi au bakteria mkubwa ni dhambi   na maelfu ya kiutendaji.

Ndoa ambayo ni uhusiano wa karibu wa familia mara nyingi ni rahisi kushambuliwa.
Mkakati uliotayarishwa na shetani mwenyewe kuingiza katika ndoa aina Fulani ya ugonjwa unao ua.

Waweza kusikiliza ushuhuda wa wazee katika ndoa zao katika sehemu ya video zetu au bonyeza hapa kwenda kwenye akaunti yetu ya youtube
 






Ndugu Eliud Misana na mke wake wakilishana keki

Dr Maeja na mke wake wakilishana keki

Mzee Kasonzo akichukua keki kwa ajili ya kumlisha mke wake ambaye hayupo katika picha kutokana na maradhi.

Mzee wa kanisa ndugu Songola na mke wake wakilishana keki


Mwalimu Magoma (mkuu wa kaya na familia) na Mke wake wakilishana keki




Mzee Geofrey Mndambi na mke wake (Wageni wa kanisa) wakiwa mbele kwa ajili ya kulishana keki. Walioana mwaka 1960 na wamekuwa msaada mkubwa kushuhudia maisha yao ya ndoa

Mzee wa kanisa ndugu Sengoka Mndambi akihubiri wakati wa huduma kuu

Ndugu Raphael na mke wake wakiwa mbele ya kanisa wakiwa katika muonekano wa kuwa pamoja kanisani

Ndugu Songola (Mzee wa Kanisa) na mke wake wakitambulishwa kanisani wakionyesha mfano wa kuwa pamoja kwa wanandoa kanisani

Mzee wa kanisa ndugu Sengoka Mndambi akitambulisha familia ya Mwalimu Magoma (Mkuu wa kaya na familia kanisani)

























Washiriki wa kanisa wakiwa katika ibada

Washiriki wa kanisa wakiwa katika ibada

Kwaya ya wanadoa wakiimba wimbo wakati ibada kuu

Mzee Mndambi na mke wake wakiimba wimbo wakati wa ibada kuu

Wanandoa wakiimba wimbo wakati wa ibada kuu

Wanandoa wakiimba kwa furaha (anayetabasamu ni mama Yuritha Nangare na anayeongoza kwaya ya wanandoa ni mzee Samweli Mboje) wakati wa ibada kuu













Ndugu Peter Stima akisoma somo la sadaka wakati wa kutoa zaka na sadaka






Share this article :

Post a Comment

 
Need Support? Contact : Creating Website and Blog | Stanley Isaac Manyonyi | Twitter
Copyright © 2017. SHINYANGA CENTRAL SDA CHURCH - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger