Home » » MTANDAO WA VITU KUBADILISHA MAISHA YAKO ZAIDI

MTANDAO WA VITU KUBADILISHA MAISHA YAKO ZAIDI

Written By SHINYANGA CENTRAL SDA CHURCH on Wednesday, May 17, 2017 | May 17, 2017

Mchungaji Musa Mika-Website and Apps Manager Ufunuo Publishing House
Kufikia mwaka 2020 inakadiriwa kuwa zaidi ya vifaa bilioni 20 hadi 100 kuunganishwa katika mtandao mmoja unaojulikana kama 'Internet of Things'. Hato yameelezwa leo na Mchungaji Musa Mika (Website and Apps Manager-Ufunuo Publishing House) wakati akiwasilisha mada ya matumizi ya machapisho ya kimtandao dhidi ya machapisho yaliyopo katika karatasi.  'Kama unadhani Intaneti imekusaidia kubadilisha maisha yako, basi jiandae kubadilishwa maisha yako zaidi kwa ujio wa mtandao wa vitu ('Internet of Things')'. Alisema Mchungaji Musa Mika.

Aliendelea kusema kuwa waumini wategemee mabadiliko ya kasi ya ulimwengu kwa sababu wanadamu wataunganishwa kwa pamoja, vitu kwa vitu vitaunganishwa na wanadamu kwa vitu pia vitaunganishwa ili kutengeneza mtandao mkubwa sana. Utakuwa ni ulimwengu ambao mwanadamu ataweza kuchemsha chai, kahawa na mabo mbalimbali akivitawala vifaa vyake vya nyumbani au ofisini akiwa mbali na maeneo yake nyumbani au ofisini.
Mchungaji Musa Mika
Wakati wa uwasilishaji alitoa faida za kutumia machapisho laini yaliyopo katika vifaa vya TEHAMA kama vile kompyuta, tabiti na simu kuweza kusoma maandiko matakatifu wakati huo huo bila kusahau kusoma ujumbe uliopo katika nakala ngumu. Aliwaomba waumini wasidharau machapisho yaliyopo katika nakala ngumu.
Wakati huo huo aliwataka waumini wawapo kanisani, kuhakikisha kuwa simu zao ziko katika hali ya utulivu wanapokuwa wakijisomea maandiko matakatifu kama vile lesoni. Pia simu ni vema iwe katika mwanga hafifu ambao hautamuathiri muumini mwenzake aliyekaribu na mtumiaji wa simu. Akisisitiza matumizi sahihi ya simu kanisani aliendelea kusema kuwa mtumiaji wa simu lazima azime sauti zote za ishara ya ujumbe wowote kuingia,hii itasaidia kutoharibu usikivu katika ibada. Kwa kuandaa apps ambazo utazitumia, itasaidia sana kuongeza usikivu.



Share this article :

Post a Comment

 
Need Support? Contact : Creating Website and Blog | Stanley Isaac Manyonyi | Twitter
Copyright © 2017. SHINYANGA CENTRAL SDA CHURCH - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger